Australia. Kadinali George Pell wa Kanisa Katoliki nchini Australia amekutwa na hatia za unyanyasaji wa kingono dhidi ya watoto.
Tukio hili linamfanya Kadinali huyo kuwa kiongozi wa kwanza mwenye hadhi ya juu kabisa wa Kanisa kukutwa na hatia hii.
Taarifa zinasema kwamba Kanidali Pell aliwafanyia unyanyasaji vijana wawili 1996, lakini amekana kuhusika.
Mashtaka yalifunguliwa tangu Desemba lakini huenda hayakuwekwa wazi kutokana na sababu za kisheria.
Pell mwenye umri wa miaka 77 anatarajiwa kuhukumiwa keshon Jumatano, lakini mawakili wake wanasema kua watakata rufaa hatia hiyo.
Hata hivyo kadinali Pell amekanusha kuhusika na matukio yote na sasa yupo katika mapumziko marefu wakati wote wa kesi hii ikiendelea.
Pell alikua katika mwaka wake wa kwanza katika kanisa la Melbourne mwaka 1996 alipowafanyia unyanyasaji watoto , baada ya kuwaambia kuwa walikunywa mvinyo wa kanisa, aliwalazimisha kumfanyia vitendo visivyofaa kama adhabu yao.
Kanisa limepata fursa ya kusikia ushahidi kutoka kwa mmoja wa waathiriwa wa unyayasaji huo, huku mwingine tayari ameshatangulia mbele ya haki.