Dar es Salaam. Wakati hali ya afya Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mhashamu Yuda Thaddaeus Ruwa’ichi ikiendelea kuimarika, jopo la madaktari leo Ijumaa Septemba 13, 2019 litakutana kuangalia uwezekano wa kumuondoa wodi ya uangalizi maalum (ICU).
Septemba 8, 2019 Askofu Ruwa’ichi alifanyiwa upasuaji wa kuondoa damu kwenye ubongo katika Taasisi ya Mifupa (Moi) na hadi leo mchana alikuwa katika chumba hicho.
Akizungumza na Mwananchi ofisa uhusiano wa Moi, Patrick Mvungi amesema jopo la madaktari saba wanaomuhudumia watakutana kuangalia hatua gani itafuta.
Mvungi amesema afya yake inazidi kuimarika na tayari ameanza mazoezi ya kukaa na kusimama.
“Kila siku asubuhi inafanyika ibada kitandani kwake na leo kwa mara ya kwanza ameshiriki akiwa amekaa, hii inaleta matumaini makubwa na anaonekana anapata nafuu kwa uharaka.”
“Kitaalam madaktari wake wanaendelea kumuangalia na watakutana kuangalia hatua gani ifuatwe apelekwe HDU au moja kwa moja aende wodi ya kawaida,” amesema Mvungi
Pia Soma
- Hukumu kesi ya DC Chemba kutolewa Septemba 18
- Waziri asema TRA ina uhaba wa watumishi 2,249
- Moto watekeleza vibanda vya wafanyabiashara Tarakea
> Magufuli amjulia hali Askofu Ruwa’ichi