Menu ›
Dini
Sun, 9 Apr 2023
Chanzo: Bbc
Unakumbuka, siku chahce zilizopita, kulitokea tukio la paka kumrukia Imam na kupanda hadi mabegani kwake wakati akiwa anaswalisha swala ya Taraweeh.
Imam huyo hakuvunja sala wala hakumshusha paka, badala yake alimruhusu paka afanye biashara yake, na yeye akaendelea na kuswalisha. Video hiyo ilisambaa katika mitandao ya kijamii duniani kote.
Imam huyo Walid Mahsas wa msikiti mmoja kule nchini Algeria ametunukiwa tuzo na serikali ya Algeria chini ya ofisi ya masuala ya dini kwa kuonyesha kwake ile picha ya Uislmau ya huruma na upendo kwa wanyama.
Chanzo: Bbc