Dalai Lama, kiongozi wa kiroho wa Tibet, ameomba msamaha Jumatatu kwa mvulana mdogo kwa kumtaka "kunyonya ulimi wake" wiki chache zilizopita wakati wa kusikilizwa kwake ambapo video ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ikiwa na kuzua hisia mbalimbali.
"Kiongozi wa kiroho wa Tibet angependa kuomba radhi kwa mvulana huyo na familia yake, pamoja na marafiki zake wengi duniani kote, kwa maumivu yoyote ambayo maneno yake yaliweza kusababisha," kulingana na taarifa iliyowekwa kwenye akaunti yake rasmi ya Twitter.
"Kiongozi wa kiroho wa Tibet huwakejeli watu anaokutana nao kwa njia isiyo na kuchukiza, hata hadharani na mbele ya kamera", amesema kiongozi huyo.
Mtazamo wa Dalai Lama 'waghadhabisha' wengi
Katika video ya tukio hilo, ambalo imesambaa mitandaoni, Dalai Lama mwenye umri wa miaka 87 alimtolea ulimi mtoto huyo ambaye alishikwa na mshangao, baada tu ya kumuuliza: "unaweza kunyonya ulimi wangu?", na hivyo kuzua kuzua hidia mbalimbali.
Video hiyo ilirekodiwa mnamo Februari 28, wakati Dalai Lama alipokuwa akifanya mkutano huko McLeod Ganj, nje kidogo ya Dharamsala, kaskazini mwa India, ambapo ameishi uhamishoni tangu kushindwa kwa uasi wa Tibet wa 1951 dhidi ya mamlaka ya China.
Watumiaji wa mtandao waliuita mtazamo wake wa "kuchukiza" na "usiofaa kabisa".