Dar es Salaam. Mtu anayedaiwa kumuua Mariam Charles (22), mwanakwaya wa Kanisa la AICT, Chang’ombe amekamatwa leo Jumamosi Septemba 8, 2018.
Mtu huyo amekamatwa wakati ibada ya mazishi ya Mariam ikiendelea baada ya kuonekana akirandaranda nje ya kanisa hilo.
Hayo yameelezwa na mchungaji kiongozi wa AICT Chang’ombe, Elisha Isebuka kabla ya kuanza kuhubiri.
“Wakati ibada inaendelea mliona baadhi ya viongozi wakitoka. Kijana anayedaiwa kufanya mambo haya alikuwa akizungukia maeneo haya na sasa amekamatwa. Tuviache vyombo vya dola vifanye kazi," amesema.
Mwili wa Mariam ulikutwa kwenye nyumba ya wageni ya East London, Buza anakodaiwa alikuwa na mchumba wake usiku wa kuamkia Septemba 5, 2018.
Soma Zaidi:
·Sakata la mwanakwaya kufia gesti, ndugu watumiwa meseji za vitisho