Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega leo Septemba 3, 2023 ameanza ziara mkoani Mwanza kwa lengo la kukagua maendeleo ya sekta za mifugo na uvuvi. Waziri Ulega ataendelea na ziara hiyo mpaka kesho Septemba 4, 2023.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega leo Septemba 3, 2023 ameanza ziara mkoani Mwanza kwa lengo la kukagua maendeleo ya sekta za mifugo na uvuvi. Waziri Ulega ataendelea na ziara hiyo mpaka kesho Septemba 4, 2023. Akiwa mkoani humo, Mhe. Ulega atakagua maendeleo ya ujenzi wa Boti na Vizimba ambavyo vitagaiwa kwa wavuvi, atatembelea maabara ya uvuvi na kufanya mikutano ya hadhara na Wananchi.