Tabora. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Makazi nchini Tanzania, William Lukuvi amepongezwa kwa kukitangaza vema Chuo cha Ualimu Tabora kwa vile ni tunda lake.
Akimzungumzia waziri huyo leo Alhamisi Oktoba 3, 2019 katika Jubilee ya miaka 50 ya chuo hicho, Mkuu wa chuo hicho, Sista Agnes Awaki amesema Lukuvi alikuwa mwanachuo aliyeingia mwaka 1968 na kumaliza 1969 akisomea astashahada ya Ualimu.
Ameeleza Waziri Lukuvi pia alikuwa miongoni mwa wanachuo waliosoma wakati chuo kikitoa mafunzo ya Kijeshi kuanzia mwaka 1975 hadi 1992 yalipositishwa.
Sista Agnes amesema wanajifunza kutoka kwake kujiendeleza na kuchapa kazi kwa umahiri na umakini mkubwa kwa kutoa mfano wa utendaji wake wa kazi kuwa unawabeba wao kama chuo.
"Tunatembea kifua mbele kutokana na uchapakazi wako mkubwa ukiwa ni zao la chuo chetu," amesema
Amewataka wanachuo na wahitimu wa chuo hicho, kuiga mazuri yote yanayofanywa na waziri huyo ambaye wanamchukulia kama kiongozi aliyetukuka.
Pia Soma
- Waziri Lukuvi apongezwa kuwa mwanafunzi bora
- Bunge Israel laapishwa bila matumaini ya Serikali kuundwa
- Nchimbi, Molinga wapiga shoo ya kibabe Yanga, Polisi Tanzania sare