Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waziri Bashungwa atoa maagizo kwa viwanda vya Arusha

67738 Pic+bushungwa

Mon, 22 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Waziri wa Viwanda na Biashara wa Tanzania, Innocent Bashungwa  amevitaka viwanda vya A to Z na Sunflag vilovyopo jijini Arusha kutengeneza vifungashio vya bidhaa za wajasiriamali wadogo ili kuwasaidia kupata masoko na kukuza biashara zao.

Akizungumza baada ya kutembelea viwanda hivyo jana Jumapili Julai 21,2019, Waziri Bashungwa  alisema wafanyabiashara wadogo  wanauhitaji mkubwa  wa vifungashio  vya bidhaa zao.

"Katika bidhaa ambazo mnatengeneza mnaweza pia kutengeneza vifungashio vya wajasiriamali wadogo kwani kuna uhitaji mkubwa" alisema.

Hata hivyo, waziri huyo alieleza kuridhishwa na utendaji wa viwanda hivyo ambavyo vimesaidia  kutoa ajira kwa vijana wengi katika jiji la Arusha.

Mkurugenzi wa kiwanda cha A to Z, Jayant  Shah alisema wanaunga mkono wazo la  waziri huyo kwa kufanya jitihada ya kutengeneza vifungashio vitakavyokidhi mahitaji ya wafanya biashara wadogo.

"Niwazo zuri ambalo waziri amelitoa tuko tayari kulifanyia kazi," alisema

Pia Soma

Meneja wa kiwanda cha Sunflag Harun Mahundi alisema anapenda Serikali ya Tanzania isititizie ubunifu na kufanya kazi kwa weledi kwa vijana ili kuongeza uzalishaji.

Mahundi aliomba pia Serikali kulegeza masharti kwa wataalamu kutoka nje ili waje nchini jambo linalosaidia kuongeza ujuzi kwa Watanzania.

Viwanda vya A to Z na Sunflag ni viwanda vya muda mrefu mkoani Arusha vikijihusisha na utengenezaji wa nguo, vyandarua, nyavu za uvuvi na bidhaa nyingine mbalimbali.

Chanzo: mwananchi.co.tz