BARAZA la Wazee Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya limewasihi wazee kuacha tamaa ya kuoa mabinti baada ya wake zao kuzeeka kwa kuwa kufanya hivyo wanahatarisha maisha kutokana na maradhi ukiwemo upungufu wa kinga mwilini (Ukimwi).
Katibu wa Baraza la Wazee Wilaya ya Mbarali, Hezron Kapwela ametoa ushauri huo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika kikata katika Kijiji cha Azimio Mswiswi Kata ya Kongolo wilayani Mbarali.
Kapwela alisema kumekuwa na tabia ya wazee kuongeza mke baada ya wake zao wa awali kuzeeka au kufariki dunia.
“Ukiangalia picha za ujana wako utaona ulikuwa na nywele zote nyeusi tiii...lakini leo hii ukijiangalia kwenye kioo utaona kichwa chote ni kama kimemwagiwa unga.