Chalinze. Watu wawili wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa sehemu mbalimbali baada ya magari mawili mizigo kugongana uso kwa uso na kisha kushika moto katika kijiji cha Mwidu kata ya Mdaula Halmashauri ya Chalinze mkoani Pwani leo asubuhi,
Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Wankyo Nyigesa amewataja waliofariki dunia kuwa ni Ally Kiara (40) dereva wa moja ya magari hayo na mtu mwingine ni mwanaume ambaye bado jina lake
Nyigesa ameeleza kuwa miili ya marehemu hao imepelekwa kuhifadhiwa katika hospitali teule ya rufaa ya mkoa wa Pwani Tumbi kusubiri ndugu kwa utambuzi na hatua zingine za mazishi.
Kamanda huyo pia amewataja majeruhi wa ajali hiyo ni Ramadhani Idd (28) na Yasini Abdalah (24) wote wafanyabiashara na wakazi wa Dar eslaama na wamelazwa katika kituo cha afya Chalinze kwa matibabu zaidi.
"Tunaendelea kujaribu kuzima moto eneo la tukio , lakini athari za awali ni magari hayo yameharibika, vifo na majeruhi kama nilivyokueleza, tunafanya uchunguzi zaidi wa chanzo cha ajali,"amesema Kamanda Nyigesa.