Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watuhumiwa watatu kortini kwa kulawiti, kumuua mtoto miaka 7

Bambeee Jela kwa kuua mfanyabishara wa madini

Tue, 21 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Watuhumiwa watatu ambao ni Mathias Shilole (26) Mkulima, Sita Makabila (52) Mganga wa tiba asili na Mkazi wa Kilimanjaro Nyangwale, na Lucy Mdelema wamefikishwa Mahakamani kwa kosa la kumuua Mtoto Dorcas Mathias mwenye umri wa miaka 7 Mwanafunzi wa chekechea Shule ya Msingi Ibambila Wilayani Nyahg"wale Mkoani Geita.

RPC wa Geita, Henry Mwaibambe amesema Watu hao watatu walimvamia Binti huyo aliyekuwa akichunga mbuzi na mwenzie na wakaondoka nae na kisha kumficha sehemu isiyojulikana na baadaye Watuhumiwa Wanaume wakambaka na kumlawiti na kumvunja shingo yake baada ya kumuua .

Mwaibambe amesema baada ya mwili huo kufanyiwa uchunguzi wa Daktari ulibainika kuwa Dorcas alibakwa, kulawitiwa na kisha kuuawa na baadaye akavunjwa shingo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live