Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Abdulaziz Abood ameongoza mamia ya wananchi wa Kata ya Lukobe kwenye mazishi ya watoto wawili wafamilia moja waliopoteza maisha baada ya moto kuteketeza nyumba waliyokuwa wamelala usiku wa Mei 4, 2024.
Watoto hao wakiume ni Brown George Banzi mwenye umri wa miaka saba na mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya Msingi Msamvu A na Bright George Banzi mwenye umri wa miaka minne na mwanafunzi wa shule ya awali
Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa Kibao cha Shule Tushikamane, Kata ya Lukobe, Omary Hassan amesema kuwa wakati nyumba hiyo inaungua moto wazazi wote wawili hawakuwapo nyumbani.