Thu, 16 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watoto watatu kutoka Kata ya Tinde Wilaya ya Shinyanga wamefariki dunia baada ya kutumbukia katika bwawa lililopo eneo la Ngaka.
Tukio hilo limetokea leo Mei 16, 2024 saa nne asubuhi katika Kijiji cha Nyambuhi ambapo watoto hao walienda katika bwawa hilo kwa lengo la kuogelea.
Jeshi la Zimamoto na Uokaji kwa kushirikiana na wananchi wamefanikiwa kupata mwili wa mtoto mmoja huku juhudi za kutafuta miili mingine ya watoto wawili zikiendelea.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live