Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wataalam wa anga Tanzania waanza uchunguzi ajali ya ndege iliyoua wawili

70162 Ndeg2+pic

Tue, 6 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Tabora. Wataalamu wa anga kutoka jijini Dar es Salaam wameanza uchunguzi wa ajali ya ndege iliyoanguka Jumamosi Agosti 3, 2019 wilayani Sikonge Mkoa wa Tabora na kusababisha vifo vya watu wawili.

Ndege hiyo yenye usajili  ZU-TAF aina ya SLG4 ilikuwa ikiruka kutoka kiwanja cha ndege cha Tabora kuelekea kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Lilongwe, Malawi. Ilianguka muda mfupi baada ya kuruka.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne Agosti 6, 2019 mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Peres Magiri amesema wataalam hao wamewasili  juzi na jana wameanza uchunguzi wao kwenye eneo la ajali.

Amebainisha kuwa bado hajaonana na wataalam hao kutokana na kushiriki ufunguzi wa maonyesho ya Nanenane Kanda ya Magharibi.

Awali ilielezwa kuwa chanzo cha ajali  hiyo ni hitilafu ya injini, rubani alitoa taarifa katika kituo cha kuongozea ndege jijini Dar es Salaam na mara baada ya taarifa hiyo ndege hiyo ilipoteza  mawasiliano na kuanguka.

Miili ya watu hao, Desmond Roy Werner (rubani) na Werner Froneman (mhudumu) lihifadhiwa katika Hospitali ya Kitete,  Tabora.

Habari zinazohusiana na hii

 

Chanzo: mwananchi.co.tz