Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wastaafu TFS waambiwa mlio wa ATM unachanganya wengi

74419 Tfs+pic

Thu, 5 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa bodi ya ushauri ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Brigedia Jenerali Mbaraka Mkeremy amewataka wastaafu wa taasisi hiyo kutumia vizuri fedha zao za kiinua mgongo ili kuepuka kudhalilika.

Amesema wasipokuwa na nidhamu hata fedha wanazolipwa kama kiinua mgongo zitakwisha na wataishia kudhalilika kama inavyowatokea wastaafu wengi nchini.

Mkeremy ameyasema hayo leo Alhamisi Septemba 5, 2019 mjini Morogoro wakati wa mafunzo ya kujiandaa na maisha baada ya kustaafu kwa watumishi 69 kati ya 78 wa TFS wanaotarajiwa kustaafu kuanzia 2019 hadi Agosti 2020.

“Mimi sijastaafu hivyo sitaweza kuwafunza kuhusu maisha baada ya kustaafu ila ninachoweza kuwaambia mimi naupenda sana ule mlio unaotoka kwenye ATM hasa ukisikika kwa muda mrefu, utasikia paraaaaaaaah nina uhakika nanyi mnapenda mlio huo.”

“Niwakumbushe kuwa na nidhamu na fedha mtakazo kwenda kupata kama kiinua mgongo licha ya wingi wake, msipokuwa na nidhamu ya fedha zitaisha na kisha kudhalilika,” anasema

Kwa upande wakem, Kamishna wa uhifadhi Profesa Dos Santos Silayo amesema wametoa mafunzo hayo kwa kuwa TFS inatambua mchango wa watumishi hao kwa usalama na uhai wa rasilimali za misitu.

Pia Soma

Advertisement
“Mchango wenu ni mkubwa katika usimamizi endelevu wa rasilimali za kitaifa za misitu na nyuki ili kuchangia mahitaji ya kijamii, kiuchumi, kisaikolojia na kiutamaduni kwa kizazi cha sasa na kijacho”

“Kutokana na mchango huo tumeamua sisi kama taasisi kuwatunuku vyeti mwaka huu, vyeti hivyo vitaambatana na kishika mkono,” amesema Profesa Silayo

Chanzo: mwananchi.co.tz