Wakazi wanaoishi nyumba za kupanga wilayani Hanang mkoani Manyara wameiomba Serikali kuongea na Wenye nyumba kutowafukuza wapangaji hao hasa katika kipindi hiki Cha Janga lililowakumba
Moses John Mbaga ni mmoja kati ya wapangaji ambaye anakutana na adha hiyo huku akisema kuwa wenye nyumba wanadai nyumba zao kuharibiwa wakati wapangaji hao wakijaribu kujiokoa huku Wenye nyumba wakitumia njia hiyo kuwaondoa
Pia amesema kuwa katika kipindi hiki watu wengi wamepoteza pesa kupitia biashara zao kusombwa na Maji na kukosa pesa ya kulipa Kodi hivyo wameiomba Wenye nyumba wawavumilie katika kipindi hiki Cha mpito