Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wanawake wafugaji wapewa mafunzo mabadiliko tabia nchi

WhatsApp Image 2021 04 08 At 12.56.16.jpeg Wanawake wafugaji wapewa mafunzo mabadiliko tabia nchi

Thu, 8 Apr 2021 Chanzo: ippmedia.com

Mratibu wa mradi wa mabadiliko ya tabia nchi kutoka katika baraza hilo, Grace Sikorei, amesema baraza hilo linatekeleza mradi huo katika wilaya tatu mkoani Arusha zikiwemo Ngorongoro,Monduli na Longido,lengo likiwa ni kuwawezesha wanawake wa jamii hizo kukabiliana na mabadiliko hayo.

Amesema mradi huo umejikita katika kuwafundisha juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji,uhifadhi wa mazingira na kutafuta njia mbadala ya kujiendeleza kiuchumi ikiwemo kujiunga kwenye vikundi vya kukopa na kuwekeza.

"Wahusika wakubwa wa mafunzo haya ni wanawake kwa sababu asilimia kubwa wao ndio waathirika wa mabadiliko ya tabia nchi kwani mabadiliko haya yanapotekea wanawake hulazimika kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya maji na chakula" amesema Sikorei.

Mzee wa Mila (Alaigwanani) David Shungea, amesema mabadiliko ndani ya jamii yapo ikiwemo mvua kwa sasa zimechelewa kunyesha tofauti na mwaka 2020 hali inayopelekea ukame na kusababisha mifugo kukosa chakula lakini pia mvua zinaweza kunyesha na majani yasiote.

Chanzo: ippmedia.com