Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wanaouza miche ya kahawa inayotolewa bure Halmashauri ya Moshi kikaangoni

Mon, 24 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Moshi.Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa, Mzee Mkongea Ally, ameagiza kuongezwa kwa Faini inayotozwa kwa wakulima wa Kahawa, ambao wamekuwa wakiuza miche ya zao hilo Kinyume cha taratibu.

Ally ametoa agizo hilo leo Juni 23,2019, baada ya kupokea taarifa ya mradi wa Bustani ya Kahawa, katika Halmashauri ya Moshi Vijijini, ameelezwa kuwa miche hiyo hutolewa bure na mkulima ambaye hubainika kuiuza, hutozwa faini Sh1,300 kwa Kila mche wa kahawa.

“Mmeniambia miche hii hutolewa bure bila malipo na ikionekana mtu anaiuza kwa mtu mwingine, faini yake ni Sh.1,300,mimi ombi langu, Faini hii iongezwe, ili kuweka  adhabu kali, kwa wale ambao wanauza kinyume cha utaratibu,” amesema Ally.

 

Aidha amesema, Halmashauri hutumia fedha nyingi kuhakikisha wakulima wanapata miche bora ya Kahawa, hivyo ni lazima wale ambao wanaiuza kwa maslahi yao wapatiwe adhabu kali.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Mratibu wa Kahawa Wilaya ya Moshi, Violeth Kisanga, amesema halmashauri imezalisha miche 38,000 ambayo inatosha  hekari 72, kwa mbegu za kahawa aina ya Compact.

Pia Soma

Kwa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Mwenge wa Uhuru, umefungua jengo la huduma za dharura katika Hospitali ya Kibosho, kuzindua kisima cha maji TPC na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa madarasa mawili ya Shule ya Sekondari Langasani na  kutembelea klabu ya kupiga vita rushwa ya shule hiyo.

Chanzo: mwananchi.co.tz