Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wananchi wampa Magufuli, Kigwangalla ng’ombe

63222 Pic+magufuli

Tue, 18 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Serengeti. Wakazi wa Robanda wilaya ya Serengeti mkoa wa Mara wametoa ng'ombe wawili kwa Rais wa Tanzania, John Magufuli na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla.

Ng’ombe hao wametolewa leo Jumanne Juni 18,2019 na Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Mrobanda Japani kwa viongozi hao kutokana na utendaji wao wakati wa hafla ya kutambulisha tuzo ya ubora wa  Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa wakazi wa mikoa ya Mara na Simiyu.

Japani ameomba Waziri Kigwangalla kuhakikisha timu iliyoundwa kwa ajili ya kufuatilia migogoro ya wananchi na wahifadhi iweze kufika kijijini hicho kumaliza migogoro hiyo kabla ya uchaguzi.

"Naomba wafanye kabla ya uchaguzi ili isije kuwa ni kisingizio cha kukosa kura," amesema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dk Kigwangalla amesema wizara hiyo imeanza kupitia kanuni za ulipaji kifuta machozi na jasho kwa watu wanaouawa, jeruhiwa na mazao kuliwa na wanyama.

"Wataalam katika wizara wanaendelea na mchakato huo na pia ulipaji wake utakuwa unafanyika kwa wakati,” amesema.

Pia Soma

Awali, mkuu wa mkoa wa Mara, Adamu Malima amesema wananchi wanalalamika kutolipwa kifuta jasho na machozi kwa wakati na wanapolipwa wanapata kiasi kidogo sana.

Kwa mjibu wa kanuni ya ulipaji fidia ya mwaka 2011 ekari moja inalipwa kati ya Sh100,000 na mtu akiawa analipwa Sh1 milioni.

Chanzo: mwananchi.co.tz