Visima vitatu vya maji katika Kijiji cha Lembapuli Kiteto vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 100 vimejazwa mawe na watu wasiojulikana
Akizungumza mbele ya Mbunge wa Jimbo la Kiteto diwani wa kata ya Loolera Kosei Lehinga amesema Kijiji cha Lembapuli mpakani mwa Kiteto na Kilindi ya Tanga kuna mgogoro wa mipaka uliodumu muda mrefu bila ufumbuzi ambapo hata gari la mtu binafsi liliwahi kuchomwa moto
Amesema visima vitatu vilivyochimbwa na wananchi wa eneo hilo ili kusaidia maji ya mifugo na binadamu kwa nyakati tofauti vimekuwa vikijazwa mawe na watu wasiojulikana ambapo wamemuomba mbunge kuingilia kati
Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Lembapuli Ole Lekaita ameagiza ufanyike uchunguzi wa haraka kwa nia ya kuwasaidia wananchi hao ambao juhudi zao zinafifishwa huku akisema nia ya Serikali ni njema na kutaka wakamatwe na kufikishwa kwenye mikono ya sheria wanao hujumu miradi.