Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wananchi wajitokeza kwa wingi kuipokea Dreamliner Dar

81835 Wananchi+pic Wananchi wajitokeza kwa wingi kuipokea Dreamliner Dar

Mon, 28 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mamia ya wananchi na wanachama wa CCM wamejitokeza Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) katika hafla fupi ya kupokea ndege ya pili ya Boeing 787-8 Dreamliner iliyonunuliwa na Serikali ya Tanzania.

Ndege hiyo imewasili leo saa 8:36 mchana ikitokea nchini Marekani na kupokewa na Rais wa Tanzania, John Magufuli pamoja na viongozi mbalimbali akiwemo Spika wa Bunge, Job Ndugai, mawaziri, wakuu wa mikoa na mabalozi.

Wakizungumzia ujio wa ndege hiyo, wananchi hao wamesema ndege hizo ni chachu ya kuongeza mapato ya Serikali.

"Nimefurahi sana kununuliwa kwa ndege hizi, zitasaidia kuboresha usafiri. Sasa wageni wengi watakuja nchini kwa ajili ya utalii,” amesema Henry Kissu, mkazi wa Buguruni.

Yasin Goba, mkazi wa Kigamboni amesema ndege hizo ni fahari ya Tanzania na angependa zifanye safari kwenda Uingereza, Marekani na China.

Amesema amefurahi kuona Rais Magufuli anatekeza Ilani ya CCM ya mwaka 2015 huku akijigamba kwamba chama hicho tawala kitashinda tena kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Pia Soma

Advertisement
Kada mwingine wa CCM mkazi wa Mbagala, Mariam Omary amesema ndege hizo zitaboresha maisha ya wananchi kutokana na mapato yatakayopatikana.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz