Wananchi wa Kijiji cha Pandambili wilayani Kongwa mkoani Dodoma, wameziba barabara kuu inayotoka Dar es Salaam kwenda mikoa mingine wakishinikiza serikali iweke alama za tahadhari katika eneo hilo baada ya mtoto mdogo kugongwa na gari hapo jana na kupoteza maisha.
Mashuhuda wamesema wananchi wamefunga barabara hiyo tangu saa 8:00 mchana wa jana Desemba 9, 2022, hali iliyopelekea kuwepo kwa foleni kubwa ya magari katika barabara hiyo.
Hadi sasa viongozi ikiwemo jeshi la polisi wamefika eneo hilo na wameweza kuwadhibiti wananchi na kuanza kuruhusu magari kutembea.
Juhudi za kumtafuta Mkuu wa wilaya ya Kongwa zinaendelea.