Ugumu wa maisha na kukosekana kwa Wasaidizi wa kulea Watoto kumetajwa kuwa kuwa sababu ya kusitisha masomo kwa Wanafunzi 92 kati ya 265 waliorejea masomoni baada ya kupata ujauzito shuleni chini ya Utaratibu wa Kuboresha Elimu Sekondari (SEQUIP).
Ugumu wa maisha na kukosekana kwa Wasaidizi wa kulea Watoto kumetajwa kuwa kuwa sababu ya kusitisha masomo kwa Wanafunzi 92 kati ya 265 waliorejea masomoni baada ya kupata ujauzito shuleni chini ya Utaratibu wa Kuboresha Elimu Sekondari (SEQUIP). Msimamizi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Dodoma, Anna John anasema “Takwimu hizo ni kwa Mwaka 2022 na 2023 katika vituo 9 vya Dodoma, baadhi ya sababu nyingine wanazotaja kuwakwamisha ni Wanafunzi hao kushawishiwa kurejea kwa wenza wao.”