Tue, 27 Aug 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Kigoma. Wanafunzi wamepewa mimba katika halmashauri ya Wilaya Kigoma kuanzia Januari hadi Juni, 2019.
Hayo yameelezwa na ofisa ustawi wa jamii halmashauri ya wilaya Kigoma, Penina Mbwete wakati wa mafunzo ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia yaliyotolewa kwa viongozi wa dini leo Jumanne, Agosti 27, 2019.
Amebainisha kuwa kati ya 12, watano ni wanafunzi wa shule za msingi na wengine saba wa sekondari.
"Hao 12 ndio walioripoti taarifa zao za mimba lakini inawezekana wapo wengi waliopata mimba huko vijijini lakini hawatoi taarifa, " amesema Mbwete.
Chanzo: mwananchi.co.tz