Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wamachinga Mwanza waandamana, wapora mali

Mwanza Maandamano Wamachinga Mwanza waandamana, wapora mali

Wed, 8 Feb 2023 Chanzo: Mwananchi

Wafanyabiashara wadogo maarufu kama Wamachinga wameandamana katika mitaa mbalimbali jijini Mwanza jana huku baadhi yao wakipopa kwa mawe maduka na kupora mali.

Maandamano hayo yaliyodumu kwa dakika zisizozidi 15 yalianza Saa 4:30 asubuhi leo Jumatano Februari 8, 2023 na kusababisha shughuli za kijamii na kiuchumi kusitishwa kwa muda katika barabara za Kenyatta, Nyerere, Station na Lumumba huku baadhi ya waandamanaji wakipaza sauti kupinga kuondolewa katikati ya jiji na madai ya mgambo wa jiji kuchukua bidhaa zao bila kuandikisha taarifa za wamiliki, kiwango na thamani ya mali.

Mwananchi imeshuhudia baadhi ya waandamanaji wakipora mali, hasa nguo zinazotundikwa kwenye midoli nje ya maduka.

Mali ya Wamachinga wanaotembeza bidhaa zao kwenye mikokoteni na kwa kubeba mikononi nayo ilikwapuliwa na waandamanaji hao ambao wengi walikuwa vijana wa jinsi ya kiume.

Ingawa Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Selemani Sekiete amesema ofisi yake haifahamu kiini cha maandamano hayo, mfanyabiashara eneo la Makoroboi katikati ya Jiji la Mwanza, Ezekiel John amehusisha tukio hilo na operesheni ya kuwaondoa wamachinga wanaorejea katikati ya jiji.

Chanzo: Mwananchi