Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Walinzi wa shule walilia mishahara ya miezi 10

38280 Lindipic Walinzi wa shule walilia mishahara ya miezi 10

Fri, 25 Jan 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Lindi. Walinzi wa shule za msingi za manispaa ya Lindi wanalalamikia kitendo cha kutolipwa mishahara yao kwa muda wa zaidi ya miezi 10 hadi sasa.

Malalamiko hayo yametolewa na uongozi wa walinzi hao wakati walipokuwa wanazungumza na Mwananchi ofisini kwao.

Salumu Abdallah, mwenyekiti wa walinzi hao alisema halmashauri ya manispaa  mwaka 2010 iliajiri walinzi 31 wa shule za msingi  kwa mikataba ya muda mrefu

Abdallah alisema tangu mwaka 2010 baada ya kupata ajira hizo malipo ya mishahara yao yamekuwa ya kusuasua hadi kufikia hatua ya kutolipwa kabisa.

Alisema jumla ya shilingi milioni 17 ambayo ni mishahara ya miezi 10 haijalipwa hadi sasa hali inayosababisha walinzi hao kukosa morari ya kufanya kazi.

“Unajua maisha yetu yamekuwa magumu sana kwa sasa kwani  tegemeo letu ni kazi yetu ya ulinzi,’’  alisema mwenyekiti huyo.

Kajura Robert alisema kitendo cha kutolipwa mishahara yao kinakwamisha kufanya shughuli zao za maendeleo ikiwemo kuhudumia familia na watoto wa shule

Ofisa elimu shule za msingi manispaa ya Lindi, Husseni Kitingi  amekiri kuwepo kwa deni la walinzi kutokana na kuwepo sheria ya elimu bure inayozuia wazazi kuchangia elimu.

Kitingi amewaomba walinzi hao kuwa wavumilivu wakati halmashauri ikihangaika kutafuta fedha kwa ajili ya malipo ya deni hilo ambalo litapunguzwa kulingana na hali ya kiuchumi itakavyoruhusu

 



Chanzo: mwananchi.co.tz