Walimu wa Shule ya Msingi Mayamaya Jijini Dodoma, Mallika Billa na mwenzake Mohamed Mochiwa wamesimamishwa kazi kwa tuhuma za kuwatumikisha wanafunzi kwa kuwachomesha Mkaa ambapo ni kinyume na utaratibu.
Maamuzi hayo yamechukuliwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Zaina Mlawa dhidi ya walimu hao.
Hatua hiyo imekuja kufuatia mwanafunzi mmoja kujeruhiwa kwa moto wakati akiwa katika kazi hiyo ambapo tuhuma nyingine ni kubebeshwa Magogo, kulima mashamba ya walimu kama vibarua bila ujira na kutowapa wanafunzi taarifa ya mapato ya Mazao ikiwemo Miradi ya Asali
Oktoba 20, 2023, wazazi na walezi walileta vurugu katika shule hiyo baada ya mwanafunzi wa Darasa la 6 mwenye miaka 13 kuripotiwa kuunguzwa na moto wakati yeye na wenzake walipotumwa na walimu hao kuzima moto bila usimamizi tena kwenye muda usio wa masomo.