Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakazi wa mji wa Mtwara kuendelea kusota na mgao wa maji

Wed, 28 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mtwara. Imeelezwa wakazi wa mji wa Mtwara nchini Tanzania wataendelea kukumbwa na mgao wa huduma ya maji licha ya mradi wa kuhamisha mabomba kupisha ujenzi wa barabara unaotegemewa kukamilika Agosti 30, 2019 kukamilika kwa zaidi ya asilimia 90.

Akizungumza leo Jumatano, Agosti 28, 2019 Kaimu mkurugenzi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Mtwara, Sauna Keya amesema kazi za msingi zilizokuwa zinafanyika zimekamilika licha ya kwamba umechukua zaidi ya miezi miwili kama ilivyotegemewa.

“Wananchi  watuvumilie kwa siku hizi chache zilizobaki na siku za mwanzo baada ya tarehe 30 kwa sababu bado maji yataendelea kuwa kwa mgao lakini wingi wa maji utaongezeka sio kama ulivyokuwa kwa sasa maji yalipungua kwa sababu ya mabomba yanayotoa maji uwezo wake ulipungua,” amesema Keya 

“Maji bado ni ya mgao wananchi wayatunze, mradi huu ulikuwa hauongezi vyanzo vingine vya maji zaidi ya kuhamisha mabomba kupisha ujenzi wa barabara, kwa hiyo maji tuliyokuwa tukiyatoa mwanzo ndio hayohayo tutaendelea kutoa japo siku za mbeleni tutaongeza vyanzo vya maji,” amesema

Meneja wa mradi huo, Ramadhani Chubi amesema kwa sasa wanamalizia kuunga bomba kubwa na kwamba mkandarasi tayari ameshapokea malighafi zilizokuwa zikihitajika.

Meneja biashara, Judithi Namwereni amewataka wananchi ambao hawapati maji hata kwa mgao kutoa taarifa ili kufuatilia mabomba yao kabla ya kukamilika ili kuepuka kuchimbua bomba hilo upya kuwaunganisha.

Pia Soma

“Pamoja na changamoto wananchi tunaomba walipe anka za maji wanazodaiwa ili kuongeza kuimarisha huduma ya mamlaka na kupanua mtandao kufia ambao bado hawapati huduma,” amesema Namwereni

 

Chanzo: mwananchi.co.tz