Wakazi wanaoishi maeneo hatarishi yaliyopo karibu na mabonde na sehemu zisizorasmi mkoani Ruvuma wametakiwa kuchukua tahadhari kwa kuondoka na kuhamia maeneo salama ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza majira haya ya masika.
Wakazi wanaoishi maeneo hatarishi yaliyopo karibu na mabonde na sehemu zisizorasmi mkoani Ruvuma wametakiwa kuchukua tahadhari kwa kuondoka na kuhamia maeneo salama ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza majira haya ya masika. Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Laban Thomas ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye kikao maalum na waandishi wa habari ofisi kwake.