Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waislamu watakiwa kuepuka maneno dhidi ya Rais Magufuli

9329 Maneno+pic TZW

Sat, 16 Jun 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Tanga.Waislamu wa Jiji la Tanga leo wameungana na wenzao Duniani katika swala ya Idd El Fitri huku wakionywa kutokubali kutamka maneno yanayodai kuwa  uongozi wa Rais John Magufuli umesababisha hali ngumu ya maisha.

Wameelezwa kwamba maeneo hayo hayapaswi kuzungumzwa na Waislamu kwa sababu yanapingana na maelekezo ya Mwenyezi Mungu ambaye ameelekeza kwamba wanapoona maisha  magumu wanatakiwa kujitafakari juu ya matendo yao.

Maelekezo hayo yametolewa leo Juni 15  na Sheikh Salim Bafadhili wakati akitoa hotuba ya swala ya Idd El Fitri iliyoswalishwa na Ustaadh Amin Said (Ammy) katika uwanja wa Tangamano Jijini Tanga

"Msizitukane zama hakika zama ni Allah mwenyewe,"alisema Sheikh Bafadhil wakati akinukuu maneno kutoka katika kitabu kitakatifu cha Quran

Aliwataka waislamu wasilalamikie hali ngumu badala yake wajikite katika kufanya ibada na kuepuka maovu ili Mungu awape wepesi katika upatikanaji wa riziki.

Sheikh huyo aliwataka wasilamu kusoma vyema dini yao ndipo watakapobaini kwamba hata walioishi zama za nyuma kuna wakati walikumbana na maisha magumu  baada ya kukiuka maandiko ya Mungu lakini waliporejea kwenye ibada ya kweli neema ilirejea.

Kuhusu Sikukuu ya Eid,Sheikh huyo aliwahimiza wanawake kuimarisha mema waliyokuwa wakiyafanya wakati wa mwezi wa Ramadhani ikiwamo kuvaa mavazi ya kuwasitiri ili amani na utulivu uliokuwepo uendelee.

Katika msikiti mkuu wa Ijumaa jijini Tanga,Sheikh wa baraza kuu lawaislamu (Bakwata) Mkoa wa Tanga,Juma Luwuchu aliwaeleza wasilamu kwamba Mwenyezi Mungu waliyekuwa wakimnyenyekea mwezi wa Ramadhani yupo miezi yote.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz