Wed, 5 Jun 2024
Chanzo: Mwananchi
Watu ambao idadi yao haijajulikana kwa haraka wanahofiwa kupoteza maisha, kufuatia ajali iliyotokea leo Juni 5,2024 katika mteremko wa Iwambi maeneo ya Mbembela jijini Mbeya.
Habari ambazo hazijathibitishwa na mamlaka, zinaeleza kuwa lori moja lililokuwa likishuka katika mteremko huo, lililiparamia basi dogo aina ya Coaster lenye linalofanya kazi Mbeya-Tunduma na kusababisha ajali hiyo.
Mwananchi Digital iliyopo eneo hilo limeshuhudia askari polisi, wakiwamo FFU na Zimamoto wakiendelea na shughuli ya uokoaji na kuifunga barabara kwa muda.
Chanzo: Mwananchi