Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wafugaji Ruvuma kuondolewa maeneo wasiostahili

75816041 Wafugaji Ruvuma kuondolewa maeneo wasiostahili

Sun, 13 Nov 2022 Chanzo: eatv.tv

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ameagiza wafugaji wote ambao wameingiza mifugo yao kwenye maeneo wasiostahili warudi kwenye maeneo yao ya vitalu.

Ametoa agizo hilo kwenye mkutano wa hadhara wakati anasuluhisha mgogoro wa wakulima na wafugaji wa Kijiji cha Mkongo wilayani Namtumbo uliosababisha watu wanne kupoteza Maisha.

Mkuu wa Mkoa ameagiza wafugaji wote waliongiza mifugo yao bila vibali,wapeleke mifugo yao katika maeneo yenye vitalu vya wafugaji ambapo katika Mkoa wa Ruvuma wilaya ya Tunduru ina vitalu vya kutosha kwa ajili ya wafugaji.

“Mkoa wa Ruvuma ndiyo Mkoa pekee nchini ambao umetenga vitalu kwa ajili ya wafugaji,Katika wilaya ya Tunduru kitalu kimoja kina hekari 500,hadi sasa kuna vitalu 107 ambavyo vipo wazi kwa ajili ya wafugaji’’,alisisitiza.

RC Thomas ametoa mwezi mmoja kwa wakuu wa wilaya zote kusimamia zoezi la utambuzi wa mifugo yote iliyopo kwenye maeneo yao kama ina vibali na namna vibali vilivyotolewa.

Chanzo: eatv.tv