Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wachimbaji madini waomba kuongezewa mwaka mmoja

59325 Dhahabupic

Thu, 23 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mirerani. Wamiliki na wachimbaji wa madini ya Tanzanite katika mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro Mkoa wa  Manyara  wameiomba Serikali kuwapa mwaka mmoja ili waweze kuboresha miundombinu ya migodi yao ikiwemo kuweka uzio.

Wametoa tamko hilo baada ya baadhi ya migodi yao ambayo haina uzio iliyopo kitalu D na B (Opec) kuwekewa alama ya X ikitakiwa kuondolewa,, kuvunja au kufukiwa.

Wakizungumza katika kikao kilichofanyika leo Alhamisi Mei 23, 2019 wachimbaji na wamiliki hao wameomba muda huo ili kukamilisha kuweka sawa miundombinu.

Amos Makoy amesema wengi wao hawana fedha na kuomba muda huo ili kutekeleza agizo hilo.

"Wachimbaji wadogo wanahitaji kuwa wachimbaji wakubwa baada ya kupata madini hivyo tunaomba Serikali ituongezee muda wa mwaka mmoja ili tutekeleze hilo," amesema Makoy.

Mwenyekiti wa kamati ya Tanzanite, Money Yousuph amesema wachimbaji wamegawanyika kwenye matabaka tofauti kiuchumi hivyo wanaomba mwaka mmoja wa kutekeleza hilo.

Pia Soma

Mwenyekiti wa chama cha wachimbaji madini mkoani Manyara (Marema) tawi la Mirerani, Shwaibu Mushi amesema ofisa madini mkazi ni msikivu kwani amekuwa akiwajali wachimbaji madini hasa wadogo.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz