Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wabunge wanawake Jumuiya ya Madola kukutana Arusha

Wabunge wanawake Jumuiya ya Madola kukutana Arusha

Wed, 23 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan Oktoba 27, 2019 atafungua semina ya wajumbe wa chama cha wabunge wanawake wa mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika itakayofanyika jijini Arusha.

Akizungumza leo Jumatano Oktoba 23, 2019  Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema semina hiyo itawakutanisha  washiriki 50 kutoka nchi 18 za Jumuiya ya Madola.

Nchi hizo ni Afrika Kusini, Botswana, Cameroon, Eswatini, Ghana, Kenya, Lesotho, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Nigeria, Namibia, Rwanda, Sierra Leone, Seychelles, Tanzania, Uganda na Zambia.

“Kauli mbiu katika semina hiyo ni kuboresha ushiriki wa wanawake katika michakato ya uchaguzi,” amesema.

Amesema miongoni mwa malengo ya semina hiyo ni kuboresha ushiriki wa wanawake katika mchakato ya uchaguzi ili kuongeza idadi ya wanawake katika vyombo vya maamuzi.

“Zipo changamoto nyingi zinazowakwamisha wanawake kushiriki mchakato ya uchaguzi kama wapiga kura na wagombea.  Changamoto hizo zote pamoja na namna ya kuzitatua zitajadiliwa katika semina hiyo,” amesema.

Pia Soma

Advertisement
Amesema mabalozi wa nchi 17 za Afrika, mawaziri na viongozi mbalimbali wanawake, viongozi wa dini, baadhi ya watendaji wa Serikali za mikoa, wilaya na mwakilishi kutoka Umoja wa Mataifa watashiriki.

Amesema uwakilishi wanawake katika baraza la madiwani nchini ni asilimia 30,  wabunge (36.6), mawaziri 11 kati ya 45 na majaji ni 19 kati ya 88.

Chanzo: mwananchi.co.tz