Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vijana wahimizwa uadilifu matumizi Mitandao ya Kijamii

Screenshot 20240204 075105 Google Vijana wahimizwa uadilifu matumizi Mitandao ya Kijamii

Sun, 4 Feb 2024 Chanzo: Dar24

Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi – CCM, Mkoa wa Kagera, Hamim Mahmoud amewataka Vijana Nchini kutumia kwa uadilifu Mitandao ya kijamii kwa kutangaza maendeleo yanayoendela kutekelezwa na Serikali.

Mahmoud ameyasema hayo wakati akiongea na Vyombo vya Habari kuhusu kilele cha maadhimisho ya miaka 47 ya Chama cha Mapinduzi – CCM, huku akiwasisitiza kuacha tabia ya kukashifu na mambo mengine yasiyofaa.

Amesema, kwasasa Taifa linahitaji vijana waadilifu na wazalendo, ambao watasaodia katika kupambana na usongeshaji mblele wa gurudumu la maendeleo, hivyo kuinua uchumi wao na pato la Nchi.

Maadhimisho hayo yatafikia kilele chake hii leo Februari 4, 2024 ambapo mgeni rasmi anatarajia kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa.

Chanzo: Dar24