Tue, 12 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Idadi ya vifo vilivyotokana na maporomoko ya matope, mawe na magogo kutoka mlima Hanang, imeongezeka hadi kufika 89.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Jumatatu Desemba 11, 2023, na Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi imesema hadi sasa miili 87 imeshatambuliwa na ndugu zao kwa ajili ya mazishi ila miwili bado haijatambuliwa.
Maporomoko hayo yaliyotokea alfajiri ya Desemba 3, 2023 na kusababisha majeruhi 139, kati yao 120 walisharuhusiwa na waliobaki hospitali ni 17.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live