Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

VIDEO:Waliokwama zaidi ya saa 20 mkoani Tanga waruhusiwa kuendelea na safari

Video Archive
Mon, 28 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Korogwe. Mkuu wa mkoa wa Tanga, Martin Shigella ameagiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kushirikiana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania  (JWTZ) kufanya tathmini ua ujenzi wa daraja la Mandera wilayani Korogwe Mkoa wa Tanga.

Daraja hilo limevunjika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Tanga na mikoa jirani na kusababisha mito kujaa maji na kuathiri madaraja, huku baadhi ya barabara zikiwa hazipitiki kutokana na maji kujaa.

Shigella ametoa agizo hilo leo Jumamosi Oktoba 26, 2019 baada ya kutembelea daraja hilo lililovunjika na kusababisha magari zaidi ya 300 yaliyokuwa yakitoka mikoa ya Kaskazini na nje ya nchi kuelekea Dar es Salaam kukwama.

Akizungumza na Mwananchi, Shigella amesema baada ya kuruhusu magari kupita, ameagiza Tanroads kufanya tathmini ya uboreshaji wa daraja hilo.

“Nimewataka wafanye tathimini ya ujenzi wa daraja, pia kukarabati sehemu korofi, nimewaomba JWTZ wasaidie na wamekubali,” amesema mkuu huyo wa Mkoa wa Tanga.

Shigella amewataka madereva kuwa makini na kubainisha kuwa ajali iliyotokea Wilaya ya Handeni na kuua watu ilitokana na dereva kupuuza maelekezo ya polisi.

Pia Soma

Advertisement
Abiria zaidi ya 2000 walikwama katika eneo hilo kuanzia jana saa 5 asubuhi na leo saa 11:50 jioni walianza kuvuka katika daraja hilo kwa kutembea kwa miguu huku magari yakivuka kwa zamu.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz