Thu, 2 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema ukarabati na ujenzi wa Soko Kuu la kihistoria la Kariakoo lililoungua utaanza Baada ya maadhimisho ya sikuku za Uhuru Disemba 9, 2021.
Ametoa kauli hiyo mapema Disemba 02, 2021 wakati akikabidhi hundi ya shilingi bilioni mbili kwa vikundi vya ujasiriamali vya sokoni hapo kwaajili ya kuendeleza shughuli zao za kibiashara.
Ameongeza kusema kuwa Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 28 kwaajili ya kukamilisha ujenzi na ukarabati huo ili soko hilo kongwe zaidi nchini.
Tazama video hapa RC Makalla akifafanua zaidi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live