Thu, 2 Nov 2023
Chanzo: Bbc
Katika kukomesha Biashara ya Ukahaba jijini Dar es salaam Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Saad Mtambule akifuatana na Meya wa Manispaa ya Kinondoni Songoro Mnyonge, wameendesha Operesheni Maaalum ya kukabiliana na vitendo vya ukahaba kwa kuvamia eneo maarufu ya kuendesha biashara ya ukahaba Mwananyamala ambapo watuhumiwa kadhaa pamoja na wateja wao wamekamatwa.
Katika Msako huo Wakina dada kadhaa walitiwa mbaroni huku wengi wao wakitoroka kupitia milango ya dharura iliyokuwa sehemu ya ndani ya madanguro hayo ambayo yamekuwa yakilalamikiwa na wananchi hususan wanaoishi katika maeneo hayo.
Chanzo: Bbc