Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

VIDEO: Alichokisema aliyenusurika katika ajali ya ndege

Video Archive
Thu, 8 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mmoja wa abiria wanane walionusurika katika ajali iliyotokea juzi Mafia, amesema ndege hiyo iliacha njia na kugonga ukuta wakati ikiwa katika njia ya mwendo wa kasi kuelekea kupaa.

Ndege hiyo ya kampuni ya Tropical ilipata ajali wakati ikiondoka Uwanja wa Ndege wa Mafia mkoani Pwani kuelekea jijini Dar es Salaam.

Hadi jana jioni Jumatano Agosti 7, 2019 abiria huyo, Hassan Bakari na wenzake watatu walikuwa wamelazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na Taasisi ya Mifupa (Moi) baada ya kuhamishwa kutoka Hospitali ya Wilaya ya Mafia juzi kutokana na kupata majeraha makubwa.

Watu sita kati ya tisa waliokuwa kwenye ndege hiyo walijeruhiwa na hakuna aliyepoteza maisha, kwa mujibu wa kamanda wa polisi Rufiji, Onesmo Lyanga.

Bakari, ambaye amepata majeraha ya moto usoni, mikononi, shingoni na kifuani, aliiambia Mwananchi jana kuwa wakati ndege hiyo ikishika kasi kwa ajili ya kuruka, ilihama njia na kugonga uzio.

 

Habari zinazohusiana na hii

Kwa habari zaidi soma gazeti la Mwananchi la leo Alhamisi Agosti 8, 2019

Chanzo: mwananchi.co.tz