Moshi. Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella amesema uzinduzi wa safari ya treni ya mizigo kutoka Tanga hadi Moshi mkoani Kilimanjaro utafungua fursa mpya za uwekezaji katika Mikoa hiyo.
Uzinduzi huo umefanyika leo Jumamosi Julai 20, 2019 na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa.
Shigela amesema treni hiyo mpya itapunguza gharama za usafirishaji wa mizigo kutoka Tanga hadi Kilimanjaro.
"Tunamshukuru Rais Magufuli (John- Rais wa Tanzania) kwa kuhakikisha safari za treni zinafufuliwa maana zitasaidia kupunguza gharama za usafirishaji wa mizigo ikiwemo saruji inayozalishwa kwa wingi kutoka Tanga kuja Kilimanjaro, "amesema.
Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amesema uzinduzi wa treni hiyo ni tukio la kihistoria nchini.
Pia Soma
- Kwa nini figo hushindwa kufanya kazi?
- Ulaji wa bamia kwa mwenye kisukari na faida zake
- Iran yakamata meli mbili za Uingereza