Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Utaratibu Mkoa wa Arusha kuondoa sokoni mifuko ya plastiki huu hapa

60180 Pic+arusha

Thu, 30 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Jiji la Arusha limetangaza utaratibu wa kuteketeza mifuko ya plastiki kuanzia Juni Mosi, 2019.

Akizungumza leo Jumanne Mei 28, 2019 ofisa afya na usafi wa mazingira wa Jiji la Arusha, James Lobikoki amesema wafanyabiashara wenye mifuko kuanzia kilo 500 na kuendelea wanapaswa kuipeleka dampo lililopo eneo la Murieti.

Lobikoki amesema wenye kilo chini ya 500 wanatakiwa kupeleka mifuko hiyo katika ofisi za serikali ngazi ya kata  ili kukusanywa na kupelekwa dampo kuteketezwa.

"Tunaamini wenye akiba ya mifuko watatekeleza maagizo haya ili kutekeleza agizo la Serikali kupiga marufuku mifuko hiyo,” amesema.

Akizungumzia mifuko mbadala amesema tayari wajasiriamali kadhaa wameanza kutengeneza na akawaondoa hofu wakazi wa jiji juu ya kubeba bidhaa zao.

Chanzo: mwananchi.co.tz