Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Usafi kila jumamosi mwisho wa mwezi- RC Makalla

MAKALLA 5?fit=700%2C466&ssl=1 Amos Makalla, Mkuu wa Mkoa wa DSM.

Mon, 22 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla ametangaza rasmi kuwa kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi ni siku ya usafi katika mkoa huo.

RC Makalla ameyasema hayo leo Novemba 22, 2021 alipokuwa akizindua Mkakati wa Usafi na Uhifadhi wa Mazingira ndani ya jiji hilo ikiwa ni siku chache ya zoezi la kuwapanga wafanyabiashara wadogo (Machinga) kumalizika.

Hata hivyo RC Makalla amesema licha ya kuwa Jumamosi ya mwisho wa mwezi Novemba itakuwa tarehe 27, 2021 amewaelekeza wananchi wa Dar es Salam kuanza rasmi zoezi la usafi ifikapo Desemba 4, 2021 kwakuwa taifa litakuwa likielekea maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru Desemba 9, 2021.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live