Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Upepo wajeruhi wawili, nyumba 49 na makanisa yaezuliwa Butiama

Wed, 16 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Butiama. Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Butiama mkoani Mara nchini Tanzania wameiomba Serikali kutoa elimu ya upandaji miti ili kusaidia madhara yanayotokana na upepo mkali kupungua.

Wakizungumza na Mwananchi leo Jumanne Oktoba 15, 2019 wananchi hao wamesema sehemu kubwa ya nyumba zilizoathirika na upepo mkali uliotokea usiku wa kuamkia jana Jumatatu Oktoba 14, 2019 unatokana na kutokuwapo kwa mti ya kutosha.

Yasinya Warioba mkazi wa Butiama ambaye nyumba yake imeezuliwa amesema mpaka sasa amejihifadhi kwa ndugu yake baada ya nyumba yake kuezuliwa na upepo.

Mkuu wa wilaya ya Butiama, Annarose Nyamubi amesema mpaka sasa  kuna majeruhi wawili wote ni watoto wa mwaka mmoja na wanaendelea kupata matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mara.

Amesema nyumba zaidi ya 49 na makanisa mawili yakiezuliwa na upepo mkali ulioambatana na mvua kubwa iliyotokea Oktoba 13, 2019.

Nyamubi amesema tukio limetokea usiku wa kuamkia Oktoba 14, 2019 ambapo mpaka sasa hakuna taarifa ya kifo tofauti na majeruhi hao wawili.

Pia Soma

Advertisement
"Mvua ilikuwa imeambatana na upepo mkali na watoto hao ndio tumepata taarifa kuwa wameumia na wanaendelea kupata matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mara na hali zao sio mbaya," amesema Nyamubi.

Mkuu huyo wa wilaya amesema kwa wote waliopata changamoto katika mvua hiyo tayari jitihada mbalimbali zimeshafanywa  na kila kitu kimeenda sawa.

Chanzo: mwananchi.co.tz