Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Upepo mkali na mvua wabomoa, kuharibu nyumba 43 Tandahimba

Upepooooo Upepo mkali na mvua wabomoa, kuharibu nyumba 43 Tandahimba

Tue, 22 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Upepo mkali uliombatana na mvua kubwa umebomoa na kuharibu nyumba 43 katika Kijiji cha Mambamba na Majengo Kata ya Mndumbwe pamoja na chumba kimoja cha darasa la Shule ya Msingi Namkomolela iliyopo kata ya Milongodi wilayani humo.

Akizungumza leo Jumatatu Novemba 21, 2022 mara baada ya kutembelea wananchi walipatwa na madhara hayo, Katibu Tawala Wilaya ya Tandahimba Juvenile Mwambi akiwa ameambatana na wajumbe wa kamati ya maafa wametoa pole kwa wananchi wa vijiji vya Mambamba, Majengo na Namkomolela walioathirika na uharibifu huo.

Amesema mvua iliyoleta madhara ilinyesha Novemba 15, 2022 na kusababisha athari kwa wakazi wa vijiji hivyo.

“Hii mvua imeleta madhara makubwa kwenye nyumba na makazi ya watu

ambapo nyumba 43 zimepata madhara sasa tunafanya tathmini ili kujua

ukubwa wa tatizo,” amesema Mwambi

Hata hivyo, baadhi ya waathirika Hassan Juma, mkazi wa Mambamba

alipotembelewa katika maeneo yao alisema tumepata madhara makubwa

kutokana na mvua na upepo mkali hivyo wanaimani kamati ya maafa itawasadia.

“Tunashukuru Serikali kwa kuwajali wananchi wake, kujali wananchi wake

kwa kufika na kuona hali halisi iliyojitokeza baada ya kupatwa na

maafa tumeathirika kwa kiasi kikubwa yaani hata vyakula vimelowa,

malazi hatuna lakini tunaimani na serikali yetu itatusaidia,” amesema

Juma.

Naye mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya

Tandahimba, Robert Mwanawima amewahikikishia wananchi walioathirika na mvua katika Kata ya Mndumbwe na Milongodi kuwa Serikali ipo pamoja nao na hatua za awali zimechukuliwa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live