Naibu Waziri wa Nishati Stephen Byabato, amesema hayo katika ziara ya kikazi kwenye kituo hicho cha kuzalisha umeme cha Mtera,ambacho uzalisha umeme Megawati 80 ambazo zinaingizwa katika grid ya taifa kwa ajili ya kupeleka umeme maeneo mbalimbali ya jijini Dodoma na Iringa.
Amesema, Gharama za Ujenzi wa mradi huo ni Sh. bilion saba,ambapo ujenzi wake ulisimama kutokana na sababu mbalimbali zilizonje ya uwezo wao lakini hivi sasa ujenzi huo utaendelea tena kwa kasi ili mradi huo wa REA awamu ya tatu uweze kukamilika.
“Nimekagua upanuzi wa mradi huu unaendelea vizuri,nimekagua pia mgodi na sehemu ya kutoa umeme, katika mitambo ambayo ina mapanga yanayozunguka kwa ajili ya kuzalisha umeme,” amesema Byabato.