Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uongozi MKURABITA kufanya ziara nyanda za juu kusini

Ae1c1bb824506e45b4134c38a899c91a Uongozi MKURABITA kufanya ziara nyanda za juu kusini

Mon, 25 Jan 2021 Chanzo: habarileo.co.tz

Mkurugenzi Mtendaji wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara Tanzania (MKURABITA) Dk Seraphia Mgembe amesema kamati ya uongozi ya mpango huo itaanza ziara kwa ajili ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa shughuli za urasimishaji wa ardhi na biashara katika mikoa ya nyanda za juu kusini.

Dk Mgembe amebainisha hayo Jijini Dodoma na kusema kuwa ziara hiyo inaanza leo na kukamilika Januari 31.2021.

“Kamati yetu itashiriki katika kazi mbalimbali ikiwemo zoezi la utoaji hati za hakimiliki za kimila na kumiliki Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa pamoja na kuweka jiwe la msingi la jengo la ofisi ya masijala ya ardhi katika Kijiji cha Kapya wilayani Mbarali mkoani Mbeya” amesema Mgembe.

Chanzo: habarileo.co.tz