Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uongozi Halmshauri Tarime wapewa siku saba kutoa mchanganuo wa Sh975 milioni

Mon, 22 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Tarime. Katibu Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) , Joseph Nyamuhanga ametoa siku saba kwa uongozi wa Halmashuri ya Mji wa Tarime kutoa mchanganuo namna ambavyo zaidi ya Sh975 milioni zimetumika kwenye ujenzi wa jengo la utawala la  halmshauri hiyo.

Nyamuhanga ametoa agizo hilo leo Juni 22,2019 baada ya kufanya ziara kukagua maendeleo ya ujenzi huo akisema hadi sasa kazi iliyofanyika haiendani na kiasi cha fedha kilichotolewa.

"Sasa hivi tunajenga vituo vya afya kwa Sh1.5 bilioni na kila kitu kinakamilika lakini ukiangalia hapa zimetumika karibia Sh1 bilioni ila kazi haiendani na thamani halisi ya fedha " amesema Nyamuhanga.

Nyamuhanga amesema kuwa amesikitishwa na kitendo cha halmashauri hiyo kushindwa kutuma Tamisemi mchanganuo wa matumizi ya fedha hizo tangu alipotoa agizo la kufanya hivyo miezi sita iliyopita.

 

Amesema mbali na mchanganuo huo, pia  mradi huo unatekelezwa taratibu na  kuutaka uongozi wa halmashuri hiyo kuongeza kasi ili mradi huo uweze kukamilika na hatimaye kuanza kutoa huduma kwa wananchi kama ilivyokusudiwa.

Pia Soma

 

Akitoa taarifa za ujenzi wa mradi huo, Kaimu mhandisi wa halmashuri hiyo, Ngalula Tungu amesema mradi huo hivi sasa umesimama baada ya Serikali kuu kutokupeleka fedha zilizoombwa na mkandarasi kwa mujibu  wa sheria na taratibu.

Chanzo: mwananchi.co.tz