Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ujenzi wa chelezo, meli mpya ziwa Victoria wafikia asilimia ilimia 30

Mon, 20 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mwanza. Ujenzi wa chelezo na meli mpya katika ziwa Victoria unaofanyika katika bandari Bandari ya Mwanza Kusini imekamilika kwa asilimia 30.

Ofisa mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli nchini (MSCL), Erick Hamissi amesema ujenzi wa meli hiyo itakayosafirisha abiria 1, 200 na tani 400 ya mizigo kati ya bandari ya Bukoba na Mwanza umekamilika katika hatua ya michoro, kuagiza vifaa na ukataji wa vyuma.

Akizungumza na Waandishi wa habari katika ziara ya kukagua kazi hiyo leo Mei 20, 2019, Hamissi amesema tayari Serikali imelipa asilimia 35 ya Sh89 bilioni za kutekeleza mradi huo kwa kampuni ya Gas Enter ya Korea Kusaini.

Hafla ya kutia saini mkataba wa ujenzi wa chelezo na meli hiyo ulioshuhudiwa na Rais John Magufuli jijini Mwanza Septemba 2, 2018.

Kaimu mhandisi Mkuu wa MSCL, Abel Gwamafyo amesema ujenzi wa chelezo itakayotumika kujenga meli hiyo na nyingine zitakazojengwa baadaye tayari umekamilika kwa asilimia 30.

“Ujenzi wa chelezo kwa gharama ya Sh36 bilioni ulioanza Februari mwaka huu unatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha mwaka mmoja,” amesema Gwamafyo.

Pia Soma

Kujengwa kwa chelezo na meli mpya itakayosafirisha abiria na mizigo katika ya miji ya Mwanza na Bukoba ni utekelezaji wa ahadi ya Rais John Magufuli wakati na baada ya kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Usafiri wa majini kati ya miji hiyo miwili ya mikoa ya Kanda ya Ziwa umekuwa wa kusuasua tangu kuzama kwa meli ya Mv Bukoba mwaka 1996, uchakavu na kuharibika kwa meli za Mv Victoria na Mv Serengeti zilizositisha huduma kati ya mwaka 2014 na 2015.

Chanzo: mwananchi.co.tz