Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ujenzi stendi ya Mbezi Luis Dar wafikia asilimia 20

63813 Pic+jiji

Sat, 22 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Sipora Liana amesema ujenzi wa stendi mpya wa mabasi ya mkoani ya Mbezi Luis umefikia asilimia 20 hadi sasa kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo  ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).

Ujenzi huo kwa sasa upo ngazi ya msingi unatekelezwa eneo la Mbezi Luis ulianza Januari 2019 changamoto hiyo imesababisha mkandarasi anayejenga stendi Hainan International kushindwa kutoa baadhi ya vifaa vyake vya ujenzi bandarini, hali inayochangia ujenzi huo kutokwenda na wakati.

Stendi hiyo mpya ambayo itatumiwa na mabasi ya kwenda mikoani na nje ya nchi itagharimu Sh50.9 bilioni ikijumuisha na ujenzi wa maduka makubwa, mabenki na itakuwa na huduma mbalimbali za kijamii

Sipora ameeleza haya leo Ijumaa, Juni 21, 2019 mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jafo alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi huo.

“Mheshimiwa waziri suala la VAT nimelifuatilia sana ikiwemo kwenda Hazina Dodoma, hadi sasa sijafanikiwa. Wiki iliyopita niliambiwa  kuwa kamati imeshakaa na kuidhinisha,  kilichobaki waziri atoe idhini kwa (AG) Mwanasheria Mkuu  wa Serikali ambaye atatangaza (GN) katika gazeti la Serikali. Hii ndio hatua iliyobaki.”

“Kuna vitu vingi vimekwama pale bandarini na kazi ingeweza kwenda mbali zaidi, licha ya kujitahidi. Tuna wasiwasi tukimruhusu mkandarasi anunue vitu ili baadaye arudishiwe fedha itakuwa mtihani,” amesema Liana.

Pia Soma

Kwa upande wake, Waziri Jafo ambaye ni mbunge wa Kisarawe alianza kwa kuwapongeza uongozi wa jiji hilo kuanza vyema mradi huo huku akisema ameridhika na maendeleo yake, licha ya changamoto mbalimbali.

Kuhusu VAT, Jafo amesema “Ile message (ujumbe) ulionitumia siku  mkurugenzi niliupeleka moja kwa moja kwa Dk Mpango (Philip -Waziri wa Fedha na Mipango), nilimwambia watu wangu wa Ubungo wamekwama katika VAT. Siyo mradi huu ipo mingi ikiwemo ya Benki ya Dunia, lakini nina imani atalifanyia kaz.”

Chanzo: mwananchi.co.tz